🇺🇸 Please click here to find an English version of this interview.

Wasagaji, mashoga, wapenda jinsia mbili na wabadilisha jinsia (LGBT) wanakumbwa na ubaguzi na vurugu ambazo zimesababisha madhara makubwa pamoja na ubinywaji wa haki zao za msingi. Niliwahoji wanaharakati watatu wa LGBT wa Tanzania ambao ni wanachama wa jamii hii ili kujua zaidi kuihusu. Lulu ni msagaji mwenye zaidi ya miaka ishirini, Grace ni mwanamke aliyebadilisha jinsia mwenye umri wa kati ya miaka ishirini na Baraka ni shoga mwenye umri wa miaka thelathini na nusu. Haya sio majina yao halisi, maana wanaishi Tanzania na hawahisi salama kujitokeza hadharani. Wanayopitia ni ya kuhuzunisha kwakweli. Nawashukuru kwa kuwa na ujasiri wa kuhojiwa. Natumaini kusoma kuhusu gharama ya maovu ya chuki dhidi ya wapendao jinsia moja na wabadilisha jinsia itamsaidia msomaji kuelewa umuhimu wa kupigania haki za wanaLGBT nchini Tanzania.
Continue reading “Mahojiano: WanaLGBT Tanzania”