Ukombozi wa Wanyama

Animal Liberation, a 1975 book by Australian philosopher Peter Singer, is widely considered one of the founding texts of the modern animal liberation movement. It develops a new ethics for our treatment of nonhuman animals, according to which their interests should be given the same consideration as the like interests of humans, and calls for an end to practices such as factory farming and animal testing. The book has had a lasting impact on generations of scholars and students and has influenced countless people in all corners of the world to adopt a vegan diet.

Almost half a century after its first publication, Animal Liberation is now finally available in Swahili! The book was translated by Deogratius Simba and published by Dar es Salaam-based publisher Mkuki na Nyota. It is available for purchase at the TPH Bookshop at 24 Samora Avenue in Dar es Salaam, and everywhere else where Mkuki na Nyota’s books are sold. The retail price is 30,000 TSh. If you are a student at the University of Dar es Salaam (UDSM), you can find a copy of the book at the library of UDSM’s Department of Philosophy and Religious Studies.

Continue reading “Ukombozi wa Wanyama”

Kile Unapaswa Kujua Kuhusu Mapenzi ya Jinsia Moja

Bonyeza hapa kupata mahojiano na mwanamme shoga na mwanamke msagaji kutoka Tanzania. Bofya hapa kujifunza zaidi kuhusu jinsia.

Mwelekeo wa kimapenzi ni nini?

Mwelekeo wa kimapenzi humaanisha muundo wa kudumu wa kimhemko, kimahaba, na/au mivuto ya kimapenzi kwa wanaume, wanawake, au jinsia zote. Mwelekeo wa kimapenzi unaweza kuwa wa toka kuvutiwa na jinsia tofauti tu hadi kuvutiwa na jinsia moja tu. Japokuwa, mwelekeo wa kimapenzi kwa kawaida hujadiliwa katika makundi matatu: mpenda jinsia tofauti (kuwa na mvuto kwa wahusika wa jinsia nyingine), shoga/msagaji (mwanaume anayevutiwa na wanaume/mwanamke anayevutiwa na wanawake), na mpenda jinsia mbili (mwanaume au mwanamke anayevutiwa na jinsia zote mbili; “bisexual”).

Continue reading “Kile Unapaswa Kujua Kuhusu Mapenzi ya Jinsia Moja”

Ubaguzi mubashara: kadhia ya maadili dhidi ya uwepo wa mipaka

Jaalia katika fikra zako kwamba: leo ni siku muruwa ya mwezi wa Septemba. Hakuna joto wala baridi, upepo mwanana unapepea na mawingu yanang’ara angani. Unachukua blanketi lako na kuelekea katika moja ya fukwe huru za jiji la Dar es salaam. Unajiandaa kwenda kujipumzisha ufukweni hapo na kufurahia machweo jua. Bali unapofika ufukweni mipango yako inatibuliwa bila ya kutegemea. Unaelezwa na afisa ulinzi kuwa serikali imeweka sheria mpya za matumizi ya fukwe. Unaambiwa kwamba huwezi kutumia ufukwe huo kwa vile wewe ni mtu mweusi. Watu wengine wowote wanaruhusiwa kutumia fukwe hizo isipokuwa watu weusi tu, na iwapo mtu mweusi yeyote angekaidi amri hiyo basi nguvu ingeweza kutumika. Continue reading “Ubaguzi mubashara: kadhia ya maadili dhidi ya uwepo wa mipaka”