Je, unajua tofauti kati ya utambulisho wa kijinsia, muonekano wa kijinsia, jinsia ki-anatomia, na mwelekeo wa kijinsi? Baadhi ya marafiki na mimi tumeunda kitini cha ukurasa mmoja, kulingana na Genderbread Person ya Sam Killermann, ambayo inafafanua dhana hizi kwa njia inayoweza kufikiwa na ya kuvutia. Ni zana nzuri ya kufundishia na njia nzuri ya kuanzisha mazungumzo muhimu, iwe shuleni, chuo kikuu, matukio ya kijumuiya, au warsha za utetezi. Ni bure kwa mtu yeyote kupakua na kutumia kwa madhumuni ya elimu, na kukuza uvumilivu, kuelewa, na kuthamini tofauti za binadamu.
Continue reading “Mtu na Jinsia”Tag: Swahili
Bonyeza hapa kupata mahojiano na mwanamme shoga na mwanamke msagaji kutoka Tanzania. Bofya hapa kujifunza zaidi kuhusu jinsia.

Mwelekeo wa kimapenzi ni nini?
Mwelekeo wa kimapenzi humaanisha muundo wa kudumu wa kimhemko, kimahaba, na/au mivuto ya kimapenzi kwa wanaume, wanawake, au jinsia zote. Mwelekeo wa kimapenzi unaweza kuwa wa toka kuvutiwa na jinsia tofauti tu hadi kuvutiwa na jinsia moja tu. Japokuwa, mwelekeo wa kimapenzi kwa kawaida hujadiliwa katika makundi matatu: mpenda jinsia tofauti (kuwa na mvuto kwa wahusika wa jinsia nyingine), shoga/msagaji (mwanaume anayevutiwa na wanaume/mwanamke anayevutiwa na wanawake), na mpenda jinsia mbili (mwanaume au mwanamke anayevutiwa na jinsia zote mbili; “bisexual”).
Continue reading “Kile Unapaswa Kujua Kuhusu Mapenzi ya Jinsia Moja”Jaalia katika fikra zako kwamba: leo ni siku muruwa ya mwezi wa Septemba. Hakuna joto wala baridi, upepo mwanana unapepea na mawingu yanang’ara angani. Unachukua blanketi lako na kuelekea katika moja ya fukwe huru za jiji la Dar es salaam. Unajiandaa kwenda kujipumzisha ufukweni hapo na kufurahia machweo jua. Bali unapofika ufukweni mipango yako inatibuliwa bila ya kutegemea. Unaelezwa na afisa ulinzi kuwa serikali imeweka sheria mpya za matumizi ya fukwe. Unaambiwa kwamba huwezi kutumia ufukwe huo kwa vile wewe ni mtu mweusi. Watu wengine wowote wanaruhusiwa kutumia fukwe hizo isipokuwa watu weusi tu, na iwapo mtu mweusi yeyote angekaidi amri hiyo basi nguvu ingeweza kutumika. Continue reading “Ubaguzi mubashara: kadhia ya maadili dhidi ya uwepo wa mipaka”