Sio Kitu: Kuanzisha mazungumzo ya falsafa ya haki za wanyama kwa Kiswahili

Namna tunavyowatendea wanyama inaonyesha kwa kiasi kikubwa utu wetu. Wanyama hawawezi kuzungumza lugha zetu, lakini wana uwezo wa kuhisi. Wanahisi maumivu, hofu, furaha na faraja—kama sisi. Wanathamini maisha yao, kama sisi tunavyothamini yetu.

Hata hivyo, kila siku wanyama wengi wanateseka. Katika mashamba, maabara, na shughuli za burudani mbalimbali, mara nyingi wanachukuliwa kama vitu tu—vitu vya kutumiwa, kudhibitiwa au kutupwa.

Ni kwa sababu hii kwamba tumeanzisha Sio Kitu.

Continue reading “Sio Kitu: Kuanzisha mazungumzo ya falsafa ya haki za wanyama kwa Kiswahili”

Falsafa ya Haki za Wanyama


Msimamo wa Haki za Wanyama

Wanyama wengine ambao binadamu huwatumia kwa chakula, katika sayansi, huwawinda, huwakamata, na kuwanyanyasa kwa namna mbalimbali, wana maisha yao binafsi ambayo yana thamani kwao wenyewe na sio tu kwa sababu ya matumizi yao kwetu. Sio tu kwamba wapowapo duniani, bali wanaufahamu. Wanachokipitia kina maana kwao. Kila mnyama ana maisha ambayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya kulingana na namna anavyotendewa.

Continue reading “Falsafa ya Haki za Wanyama”

First issue of Falsafa published

The Department of Philosophy at Hindu College in New Delhi just published the first issue of the first edition of its new magazine, Falsafa. Congratulations to the students who worked hard to put it together, and to their dedicated teachers, particularly my friend Dr. Krishna M. Pathak! I wish the magazine and its team of editors all success, and I hope it will continue to contribute to the free exchange of ideas at Hindu College for a very long time. Continue reading “First issue of Falsafa published”